Ziara ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Katika kuadhimisha miaka 62 ya Muungano wa Tanzania, Uongozi wa Baraza la Manispaa Magharibi ‘A’ kwa kushirikiana na viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali walishiriki katika ziara ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdalla, kwa kukagua miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba za wazee Walezo, barabara ya Mwembe Mchomeke (Mtofaani), skuli na hospital katika Kambi ya KVZ Mtoni na jengo la Wakala wa Ulizi JKU Mtoni.

Mafunzo ya Madiwani kuhusiana na Majanga na Maafa

Matukio ya mafunzo maalum ya kuwajengea uelewa Waheshimiwa Madiwani juu ya suala zima la majanga na maafa yalioandaliwa na Kamisheni ya Maafa Zanzibar yaliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Manispaa Magharibi ‘A’

Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mjini Rajab Ali Rajab ambae ni Mkuu wa Walaya ya Kati  akikabidhi Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Magharibi ‘A’ Rashid Simai Msaraka ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A na Viongozi mbali mbali wa Wilaya ya Magharibi ‘A’

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Magharibi  ‘A’ ambae pia ni Mkuu wa Walaya ya Kaskazini A  Rashid Simai Msaraka na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali wakikimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa