Vibali vya ujennzi
Vibali vya ujenzi
Vibali vya ujenzi vipo vya aina mbili :-
1) Nyumba za kawaida garama yake ni kuanzia 150,000 /= shilingi na kuendelea.
2) Nyumba za gorofa garama yake ni kuanzia 1,000,000 /= shilingi kwa kila gorofa moja.
Vitu vinavyohitajika ili kupata kibali cha ujenzi
- Fomu ya kibali cha ujenzi ada yake ni 20,000/= shilingi.
- Fomu ya sheha
- Kivuli cha hati miliki.
- Kivuli cha kitambulisho.
- Ramani ya mjengo.
Utaratibu wa vibali vya ujenzi
- Kufika katika ofisi ya mipango miji iliyopo katika ofisi ya Manispaa Magharibi "A" kwa ajii ya kuchukuwa fomu. Kabla ya kuanza ujenzi.
- Kupeleka fomu kwa sheha wa shehia.
- Kurudisha fomu katika ofisi ya mipango miji.
- Ukaguzi wa eneo unaofanya na maasifa ya mipango miji.
- Kupatiwa kibali cha ujenzi.
Wanaostahiki kukata kibali cha ujenzi
- Watu wote wanaooanza kujenga katika eneo ya Manispaa ya Magharibi "A".
- Watu ambao vibali vyao vimeisha mda wake. Kumbuka kibali cha ujenzi ni mda wa mwaka mmoja.
- Watu waliojenga zamani kabla ya ukataji wa vibali na wanaendelea na ujenzi hivi sasa.